pmbet

Watano wafariki baada ya mgodi wa dhahabu kuporomoka

Eric Buyanza

May 25, 2024
Share :

Watu wasiopungua watano wamekufa na wengine kadhaa haijulikani walipo baada ya maporomoko kutokea kwenye mgodi wa dhahabu usio rasmi kaskazini mwa Kenya. 

Watu wawili waliojeruhiwa wanapatiwa matibabu hospitalini. Kamishna wa Kaunti ya Marsabit David Saruni amesema ajali hiyo imesababishwa na  mvua kubwa zinazoendelea kunyesha.

Kiongozi wa serikali kwenye eneo hilo, Paul Rotich amesema ripoti kutoka kwa vikosi vya uokoaji, imebaini kuwa wachimbaji 8 walikuwa ndani ya mgodi huo wakati maporomoko hayo yanatokea.

pmbet
pmbet

Leagues standings

Tanzania Premier League
pmbet
pmbet