Wincate wa Yanga Princess ajiunga na Simba Queens
Sisti Herman
July 30, 2024
Share :
Klabu ya Simba Queens leo imemtambulisha rasmi beki wa kushoto wa Kimataifa wa Kenya Wincate Kaari kuwa mchezaji wao kutokea Yanga Princess.
Kama tulivyochapisha wiki iliyopita kuwa Simba Queens imekamilisha uhamisho wa wachezaji watatu wa kimataifa kutoka Yanga, Precious Christopher na Wincate wametangulia kutambulishwa huku Utambulisho wa kiungo wa kati raia wa Nigeria Marry Saiki Atunike ukifuatia.