Yanga yalamba dili la kutangaza utalii Zanzibar.
Joyce Shedrack
March 28, 2025
Share :
Klabu ya Yanga leo imesaini mkataba wa mahusiano ya ushirikiano na Kamisheni ya Utalii chini ya Wizara ya Utalii na Mambo ya Kale kwa ajili ya kutangaza vivutio vya Utalii vya Zanzibar.
Waziri wa Utalii na Mambo ya Kale Zanzibar, Mudrick Ramadhan Soraga ameshuhudia utiaji saini huo wa mkataba wa mwaka mmoja na Nusu ambapo upande wa Serikali umewakilishwa na Katibu Mtendaji Kamisheni ya Utalii Arif na upande wa Yanga Afrika umetiwa saini na Rais wa Klabu @caamil_88 pamoja na Makamu wa Rais @arafat__ah .
Mahusiano haya yatadumu mpaka mwisho wa msimu wa 2025/26.