Yanga yamsajili Shekhan kutoka JKU
Sisti Herman
December 16, 2023
Share :
Klabu ya Yanga imethibitisha kukamilisha usajili wa kiungo wa JKU Shekhan Ibrahim mwenye umri wa miaka 18 tu.
Yanga imemnasa kinda huyo kwa fedha za kitanzania milioni 60 ambazo zitalipwa kwa awamu 3, amesaini mkataba wa miaka mitatu.
Pia inaelezwa kuwa Simba ilikosa nafasi ya kumsajili kiungo huyu dakika za mwisho baada ya kuchelewa kutuma tiketi yake ya ndege.