Zaiylissa atangaza kufunga ndoa na Mr.Said.
Joyce Shedrack
February 18, 2026
Share :
Muigizaji Zaiylissa ametoa taarifa ya kuwa tayari amefunga ndoa na Mr.Said kupitia ukurasa wake wa Instagram amepost video inayomuonyesha akiwa na mume wake katika hali ya kimahaba na kusindikiza na ujumbe "ALHAMDULILAH Official Mrs Said".

Ikumbukwe staa huyo kabla ya ndoa hiyo aliwahi kufunga ndoa zingine mbili ambazo zote zilivunjika huku mojawapo aliifunga na nguli wa michezo Haji Manara ambaye kwa sasa ni diwani wa Kariakoo.





