Zanzibar yapiga bil. 2.6 kwa mwezi kupitia bima za wageni
Sisti Herman
March 15, 2026
Share :

Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar hukusanya takriban dola milioni 1 (Sh2.6 bilioni) kila mwezi kupitia bima ya lazima kwa wageni wanaoingia visiwani humo.
Mpango huo ulianza tarehe 1 Oktoba 2024 na unawataka wasafiri kulipa dola 44 kwa kila kuingia. Hata hivyo, wageni kutoka nchi wanachama wa East African Community hulipa dola 22 ili kuhamasisha ushirikiano wa kikanda.
Akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari Machi 12, 2026, Waziri wa Fedha na Mipango wa Zanzibar, Juma Malik Akil, alisema fedha hizo hutumika kugharamia huduma kwa wageni na sehemu nyingine kusaidia sekta ya afya.
Alieleza kuwa mpango huo umeanzishwa kusaidia wageni wanaokumbwa na changamoto kama matatizo ya afya wakati wa ziara zao visiwani





