Ziara ya siri ya Netanyahu nchini UAE yazua taharuki
Eric Buyanza
May 14, 2026
Share :

UAE imekanusha taarifa zinazoeleza kuwa Waziri Mkuu wa Israel, Benjamin Netanyahu, alifanya ziara ya siri nchini humo wakati wa vita kati ya Marekani, Israel na Iran.
Katika taarifa iliyotolewa na Wizara ya Mambo ya Nje ya UAE, serikali hiyo ilisema: “Umoja wa Falme za Kiarabu unakanusha taarifa zilizochapishwa kuhusu ziara ya Waziri Mkuu wa Israel au kupokea ujumbe wa kijeshi wa Israel.”
Kauli hiyo imekuja baada ya vyombo kadhaa vya habari vya kimataifa, vikiwemo Reuters na CBS News, kuripoti Jumatano kwa kunukuu Ofisi ya Waziri Mkuu wa Israel kwamba Netanyahu alifanya ziara ya siri nchini UAE wakati wa vita dhidi ya Iran na kukutana na Rais wa UAE Mohammed bin Zayed Al Nahyan.
Awali, Ofisi ya Netanyahu ilikuwa imesema ziara hiyo iliashiria “hatua ya kihistoria” katika uhusiano kati ya Israel na UAE.
Wakati huo huo, gazeti la Israel Hayom liliripoti kuwa Israel iliipatia UAE mfumo wa ulinzi wa anga wa Iron Dome wakati wa vita vya karibuni, madai yaliyonukuliwa kutoka kwa Mike Waltz ambaye alisema UAE ilionekana kutumia mfumo huo uliotolewa na Israel.
BBC





