Zuberi Foba afungiwa mechi tatu na faini ya Milioni 2.
Joyce Shedrack
July 13, 2026
Share :
Golikipa wa Azam FC Zuberi Foba amefungiwa michezo mitatu pamoja na kutozwa faini ya TZS milioni 2 kwa kumshambulia mwamuzi baada ya filimbi ya mwisho kwenye fainali ya Kombe la Shirikisho la CRDB dhidi ya Simba.





